Monday, January 13, 2014

MAOMBI KABLA YA KUFUNGA NDOA


Maandiko: Mithali 18:22, Zaburi 37:5

  • Moto wa roho mtakatifi (x3) katika jina la Yesu (x3)
  • Mungu uishiye mahari pa juu na Baba wa milele, ninakusifu na kukuabudu.
  • Imeandikwa kuwa “Apataye mke (mume) apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA “ Hivyo basi nadai upendeleo katika yote ninayofanya, katika jina la Yesu.
  • Bwana, ninakuomba utufanyie njia mimi na mwenzi wangu, Tupatie fedha na usaidizi wa kutosha wenye kuleta mafanikio katika harusi yetu, katika jina la Yesu (x3)
  • Ninamzamisha mke (Mume) wangu mtarajiwa kwenye damu ya Yesu
  • Ninampiga upofu shetani na maajenti wake ili wasimwone, katika jina la Yesu (x2)
  • Tukinge na ajari katika njia zote tutakazoziendea, katika jina la Yesu.
  • Bwana, tjalie upendeleo wa Kiungu kwa kila tutakaemwendea, katika jina la Yesu.
  • Ninakuja kinyume na Falme na mamlaka zote zilizo kinyume na harusi yetu, katika jina la Yesu.
  • Ninavuruga kila mpango wa Yule mwovu ulioandaliwa kuharibu ndoa yetu, katika jina la Yesu.
  • Ninafunga kila pepo lililoandaliwa kupinga ndoa yetu, katika jina la Yesu.
  • Baba,  ifanye harusi yetu kuwa yenye mafanikio, pokea utukufu katika jina la Yesu.

Amina.


ANGALIZO:  Funga kwa siku 2, kuanzia saa 12 alfajiri hadi 12 jioni huku ukiomba maombi haya.