MAOMBI NA MASOMO YALETAYO MIUJIZA:
KUFUNGUA MILANGO ILIYOFUNGWA
Maandiko: ufunuo 3:8, II Korint. 2:12, Malaki 3:10-12, Malaki 1:10
VIPENGERE VYA MAOMBI
- Katika jina la Yesu (Mara 3)
- Mwamba wangu wa kale, ninakuhabudu. Uinuliwe katika jina la Yesu
- Milango yote iliyofungwa ninaiamru ifunguke, katika jina la Yesu (x2)
- Ninaamru radi toka juu ibomoe kila ufunguo uliotumika kuyafunga mafanikio yangu, katika jina la Yesu (x3)
- Ninaufungua mwili wangu, nafsi na roho kutoka katika kila kifungo cha Shetani katika jina la Yesu (x3)
- Ninaamru udhihirisho wa Baraka kutoka MASHARIKI, MAGHARIBI, KASKAZINI na KUSINI, katika jina la Yesu. Amina
- Milango yote inayoingiza uchafu ninaimru ifunguke katika jina la Yesu (x3)
- Ninaizamisha biashara yangu, mali na familia yangu kwenye damu ya Yesu (x2)
- Utukuzwe Bwana kwa kuwa umeyajibu maombi yangu katika jina la Yesu.
AMINA.
2.MAOMBI DHIDI YA UCHAWI NA MASHAMBULIZI YA KICHAWI.
Vipengere vya maombi
- Moto wa Roho Mtakatifu(Rudia Mara 7), Damu ya Yesu(Mara 7)
- Baba katika jina la Yesu, ninakuja kwako nikisihi damu ya Yesu itakase nafsi yangu, roho na mwili pia.
- Imeandikwa katika Isaya 54:17 kuwa “Kila silaha itakayofanyika juu yangu haitafanikiwa”. Na ninatamka sasa kuwa kila silaha ya kichawi iliyo kinyume nami haitafanikiwa katika jina la Yesu.
- Popote pale ambako jina langu, pesa zangu ama mali zangu zimechukuliwa katika ulimwengu wa roho, ninazidhoofisha nguvu hizo katika jina la Yesu (rudia mara 2)
- Imeandikwa katika Mithali 18:10 kuwa “Jina la Bwana ni ngome imara. Mwenye haki hukimbilia na kuwa salama”. Ninadai usalama wangu sasa dhidi ya kila nguvu ya adui katika jina la Yesu.
- Ninawafunga wachawi wote wanaoshambulia maisha yangu katika jina la Yesu.
- Ninawatosa adui zangu wote kwenye moto wa roho Mtakatifu. Wakakose amani mpaka apo watakapotubu.
- Kila mshale uliorushwa kwangu, ninauzuia kwa kutumia ngao ya Roho Mtakatifu na ninauamuru uwarudie walioutuma, katika jina la Yesu.(Rudia mara 3)
- Ninanyunyizia damu ya Yesu juu ya kila kioo watakachotumia kutaka kuibua taswira yangu na ninaamuru radi kutoka mbinguni ikavunjevunje, katika jina la Yesu. (Rudia mara 3)
- Kupitia damu ya Yesu, ninafuta athari zote zitokanazo na vitu vyote vya kipepo watakavyonitupia ili nivikanyage, katika jina la Yesu.
- Hata kama wataniwekea sumu kwenye chakula changu ama kinywaji, ninaibatilisha sumu hiyo kwa kutumia damu ya Yesu. (Rudia mara 3)
- Ninaizamisha nafsi yangu, mwili na roho katika damu ya Yesu. (mara 3)
- Ninaharibu kila nguvu ya kichawi iliyoko dhidi ya maisha yangu, katika jina la Yesu. (Rudia mara 3)
- Popote na kwa yeyote yule ambaye anatumiwa na Shetani, awe ni baba yangu, mama, dada, kaka, shemeji au wifi ninawatamkia kutofanikiwa katika njia zoa, katika jina la Yesu.
- Ninaifunika familia yangu, biashara na mali zangu zote kwa damu ya Yesu. (Rudia mara 3)
- Baba, achilia malaika wako wanilinde mimi na vyote nilivyonavyo, katika jina la Yesu.
ANGALIZO: Kama mashambulizi yatang’ang’ania, funga kuanzia saa 12 alfajili hadi 12 jioni kwa siku 3 mfululizo huku ukiomba kila siku.