Maandiko:
Zabuaria 127:3, Mwanzo 1:28.
VIPENGERE
VYA MAOMBI
- Damu ya Yesu(x3); Katika jina la Yesu (x3)
- Baba wa mbinguni, Muumba mbingu na nchi, ninakuabudu. Bwana, ninayakabidhi kwako maisha yangu na ya mtoto aliyeko tumboni mwangu ili uyatawale, katika jina la Yesu.
- Maendeleo yote ya mtoto huyu ninayaacha mikononi mwako.
- Bwana, tupatie fedha mimi na mume wangu ili tuweze kumlea na kumtunza mtoto huyu, katika jina la Yesu.
- Ninaagiza moto wa Roho Mtakatifu uteketeze kila mkono mbaya utakaogusa tumbo hili kwa lengo la kuharibu ujauzito huu, katika jina la Yesu (x3).
- Ninalipiga upofu kila jicho lenye hila dhidi ya mtoto wangu, katika jina la Yesu (x3)
- Ninabatilisha kila shambulizi la kipepo dhidi ya mtoto wangu, katika jina la Yesu (x3).
- Popote pale ambapo kuna wachawi wanaopanga kumchukua mwanangu, ninafutilia mbali jitiada zao hizo na kuamru moto wa Roho Mtakatifu uwateketeze hadi pale watakapomwaachia mwanangu, katika jina la Yesu.
- Ninaharibu kila hali za Shetani na mawakala wake huko hospitalini, nyumbani, au popote pale, ambazo zimeandaliwa kunizuia nisijifungue salama, katika jina la Yesu (x3).
- Ninajizamisha damuni mwa Yesu mimi na mwanangu, katika jina la Yesu (x3).
- Ninatamka na kudai usalama wa maisha yangu na mwanangu aliyeko tumboni, katika jina la Yesu(x3).
- Ninaifunika kwa damu ya Yesu nyumba yangu pamoja na hospitali nitakayokwenda kujifungulia (itaje jina).
- Ninatamka kuwa manesi na madaktari wa hospitali hii (itaje jina) watafanyika vyombo vya Mungu vitakavyonisaidia nijifungue salama. Katika jina la Yesu.
- Asante Bwana kwa kuyajibu maombi yangu, katika jina la Yesu.